Thursday 5 October 2017

FURSA ZILIZOPO MKOA WA KAGERA KATIKA SEKTA YA UVUVI.

Mkoa wa Kagera una eneo la maji lenye ukubwa wa kilomita za mraba 10,655 sawa na asilimia 27, jiografia nzuri, maeneo chepechepe yenye udongo unaotunza maji na vyanzo vingi vya maji (water bodies) kama vile mto Kagera, Mto ngono, mto Ruvuvu, mto Kanoni, Ziwa Victoria na maziwa mengine madogo madogo 15. Mkoa huu wa Kagera unasifika na kuwa Mkoa wa kwanza nchini Tanzania na wa pekee wenye maziwa madogo madogo (Satellite Lake) mengi yanayofikia 15 kama yafuatayo.

Ziwa Burigi Ziwa Burigi linapakana na Wilaya tatu ambazo ni Muleba, Karagwe na Biharamulo Mkoa wa Kagera. Ziwa hili lina samaki wengi aina ya Sato (Oreochromis esculentus), Furu (Haprochromis), Kamongo (Protopterus) na Kambale (Clarius gariepinus). Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Rwakajunju Ziwa Rwakajunju linapatikana Wilaya ya Karagwe Mkoa wa Kagera. Ziwa hili lina ukubwa wa km2 27.72. Baadhi ya samaki waliomo ni pamoja na Furu (Haprochromis), Sato (Oreochromis esculentus na Variabilis), Kamongo (Protopterus) na Kambale (Clarius gariepinus). Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni pamoja na Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Kamakala Ziwa kamakala linapatikana Wilaya ya Karagwe Mkoa wa Kagera. Ziwa hili linasifika kwa kuwa na samaki wengi aina Sato (Oreochromis esculentus), Furu (Haprochromis), Kamongo (Protopterus) na Kambale (Clarius gariepinus). Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Ikimba Ziwa Ikimba linalinapatikana Wilaya ya Bukoba Mkoa wa Kagera. Ziwa hili lina ukubwa wa km2 38.09. Baadhi ya samaki waliomo ni pamoja na Furu (Haplochromines), Sato (Oreochromis esculentus), Kamongo (Protopterus catastoma) na Kambale (Clarius gariepinus). Ziwa hili linapatikana Bukoba Vijijini Mkoa wa Kagera. Baadhi ya changamoto zilizopo Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Rushwa Ziwa Rushwa linapatikana Wilaya ya Kyerwa Mkoa wa Kagera. Ziwa hili lina ukubwa wa km2 10.08. Baadhi ya samaki waliomo ni pamoja na Sato (Oreochromis esculentus, leocosticus, niloticus, variabilis na Tilapia zilii), Kamongo (Protopterus aethhiopicus) na Kambale (Clarius gariepinus). Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni pamoja na Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Melula Ziwa Melule liko Wilaya ya Kyerwa Mkoa wa Kagera. Ziwa hili lina ukubwa wa km2 15.21. Samaki waliomo ni pamoja na Sato (Oreochromis esculentus na niloticus), Furu (Haplochromines) na Kambale (Clarius gariepinus). Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni pamoja na Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Katwe  Ziwa katwe linapatikana Wilaya ya Kyerwa Mkoa wa Kagera. Ziwa hili lina ukubwa wa km2 2.23. Ziwa hili lina aina 6 za samaki ambao ni pamoja na Sato (Oreochromis leocostictus), Furu (Haprochromines), Kamongo (Protopterus aethiopicus), Kambale (Clarius gariepinus), (Momyrus) na Gogogo (S.afrofischeri). Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Luko Ziwa Luko linapatikana Wilaya ya Kyerwa Mkoa wa Kagera. Ziwa hili lina samaki wengi aina nyingi ya Sato (Oreochromis esculentus), Kamongo (Protopterus) na Kambale (Clarius gariepinus). Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni pamoja na Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Kalenge Ziwa Karenge linapatikana Wilaya ya Kyerwa Mkoa wa Kagera. Ziwa lina aina 9 za samaki ambao ni Sato (O.leocostictus, niloticus na variabilis), Furu (Haplochromines), B.profundus na B.sadleri, Kambale (Clarius gariepinus na C.alluaudi) na Gogogo (S.afrofischeri). Ziwa hili linakumbwa na changamoto ya Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumu na magugu maji.

 Ziwa Mitoma Ziwa Mitoma linapatikana Wilaya ya Kyerwa Mkoa wa Kagera. Kuna aina 5 za samaki ambao ni (B.sadleri), Kambale (Clarius gariepinus), Furu (Haplochromines), Kamongo (Protopterus aethiopicus) na Gogogo (Synodontis afrofischeri).

Ziwa Kaburi Ziwa Kaburi linapatikana Wilaya ya Karagwe Mkoa wa Kagera. Ziwa hili linasifika kuwa na samaki wengi aina Sato (Oreochromis esculentus), Kamongo (Protopterus aethiopicus) na Kambale (Clarius gariepinus). Baadhi ya changamoto zilinazopo ni Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na kilimo na magugu maji.

Ziwa Kitete, Ziwa Kitete linapatikana Wilaya ya Karagwe Mkoa wa Kagera. Ziwa hili linasifika kwa kuwa na samaki wengi aina Sato (Oreochromis esculentus), Furu (Haplochromines), Kamongo (Protopterus) na Kambale (Clarius gariepinus). Ziwa hili Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni pamoja na Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Kabindi Ziwa Kabindi linapatikana Wilaya ya Karagwe Mkoa wa Kagera. Ziwa hili linasifika kwa kuwa na samaki wengi aina Sato (Oreochromis esculentus), Furu (Haplochromines), Kamongo (Protopterus) na Kambale (Clarius gariepinus). Ziwa hili Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni pamoja na Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Ngoma Ziwa Ngoma linapatikana Wilaya ya Karagwe Mkoa wa Kagera. Ziwa hili linasifika kwa kuwa na samaki wengi aina Sato (Oreochromis esculentus), Furu (Haplochromines), Kamongo (Protopterus) na Kambale (Clarius gariepinus). Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni pamoja na Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Rumanyika Ziwa Rumanyika linapatikana katika hifadhi ya rumanyika Wilaya ya Kyerwa. Ziwa hili linasifika kwa kuwa na samaki aina Sato (Oreochromis esculentus), Furu (Haplochromines), Kamongo (Protopterus) na Kambale (Clarius gariepinus).

No comments:

Post a Comment