Thursday 8 November 2018

EMPEFU

Hii ni aina nyingine ya uyoga wa asili unaopatikana wilayani kwetu Muleba, Ukiwa maeneo ya Muleba mjini Eneo liloongoza kwa upatikanaji wake  ni KASHAKO na huu ndo msimu wake Hivyo wale mnaotembelea mashambani usikipite kichuguu bila kutupia jicho.

Kwa wale msio ifahamu KASHOKO
Hii ipo KATA YETU YA MULEBA BUKONO Maarufu kama KASHAKO AU KISHENYI pana historia yake. Zamani walichimba udongo maeneo hayo alafu wanausiliba ukutani kama lip wengine wakitumia nyasi ambazo zimeshakariwa ndani ya nyumba na kutupwa shambani mabaki yake (Esingo) udongo huu una kuwa na rangi ya Majivu ukisha kauka wakati mwingine unaweza dhania imechanganywa na cement kwa uzuri wake but ni zamani KIDOGO na asiri inapotea.

TUKUTANE DECEMBER 25
#mulebamiamia
Kizalendo Zaidi.

No comments:

Post a Comment